StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

June 27, 2012

DROGBA HUENDA AKATUA BARCA

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
DIDIER Drogba anaweza kufanya uhamisho wa kushangaza kuhamia Barcelona ya Hispania ikiwa ni muda mfupi tangu kusaini mkataba wa kuichezea timu ya  Shangha Shenhua ya China.
Nyota huyo wa Ivory Coast, aliachana na klabu yake ya Chelsea aliyoiwezesha kutwaa taji la Klabu Bingwa Ulaya na kuamua kwenda China.
Alitarajia kwenda mjini Barcelona kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Wakurugenzi wa klabu hiyo. Mazungumzo hayo yalipangwa kufanyika Jumanne wiki hii.
Drogba (34) alitarajia kulipwa mshahara wa pauni 200,000 (Sh483 Milioni) kwa wiki na klabu hiyo ya China.
Aliposaini alisema: "Nathibitisha nimesaini kucheza klabu ya Shanghai Shenhua ya China kwa miaka miwili na nusu. Nitarejea kujiunga na klabu Julai.
"Nimetafakari ofa zote nilizopewa wiki kadhaa zilizopita, lakini nadhani Shanghai Shenhua ni sehemu sahihi kwangu kwenda kwa muda huu.
"Najiandaa kukutana na changamoto mpya na kujifunza utamaduni mpya pia. Lakini pia nafurahia kusikia maendeleo ya Ligi Kuu China.
"Chelsea ilipokwenda China mwaka jana, tulikuwa na fursa nzuri na mashabiki walitufurahia. Natarajia kuitangaza ligi ya China duniani kote," alisema Drogba.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat