StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

June 27, 2012

HODGSON: NAKIRI ROONEY ALIPWAYA EURO

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
KOCHA Roy Hodgson amesema mshambuliaji wake, Wayne Rooney alishindwa kutimiza matarajio ya mashabiki wa England kwa sababu hakuwa fiti, lakini akasisitiza hali hiyo siyo sababu kubwa ya England kutolewa kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya.

Hodgson alisema alifahamu matarajio ya wengi kutaka kumuona Rooney akicheza kwenye kiwango cha juu baada ya kushindwa kucheza mechi mbili za kwanza kutokana na kukabiliwa na adhabu aliyopewa kwa kosa alilofanya Oktoba mwaka jana, kwenye mchezo dhidi ya Montenegro.
Lakini baada ya kufunga bao la ushindi dhidi ya Ukraine, Rooney alikuwa chini ya kiwango kwenye mchezo wa robo fainali dhidi ya Italia na kufungwa kwa mikwaju ya penalti 4-2 baada ya dakika 120 za mchezo uliomalizika bila kufungana mjini Keiv.
Hodgson alisema: "Tatizo tuliweka matarajio mengi kwa Wayne.
"Alipokosa michezo miwili ya kwanza, tuliamini mchezo wa tatu, Wayne Rooney atatupeleka kwenye ubingwa.
"Nadhani matarajio yalikuwa zaidi ya uwezo wake pamoja na kwamba alijitahidi. Hakucheza kwenye kiwango chake. Nadhani hata yeye atakiri hali hiyo."
Aliongeza: "Tuweke matumaini makubwa kwa Rooney? Sawa nakubali, lakini timu zingine zina wachezaji pia, si ndiyo? "Nadhani kama (Andrea) Pirlo angecheza vibaya usiku ule, angegharimu kiwango kilichoonyeshwa na Italia."
"Nafikiri timu zote kubwa kuna wachezaji wawili, au watatu ambao kila mmoja anawatambua kwa michango yao kwenye timu.
"Unapokuwa kwenye mashindano unategemea wachezaji hao wataonyesha kiwango kuthibitisha ubora wao kama ilivyowahi kutokea kwa Maradona aliyeiwezesha Argentina kutwaa ubingwa wa dunia."
Rooney alikwenda mapumziko Las Vegas, Marekani mara baada ya ligi ya England kumalizika na alipigwa picha akijirusha kwenye klabu ya usiku mida ya alfajiri.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat