
Brandts kulia akiwa na Saintfiet wakati wa Kagame
Na Mahmoud Zubeiry
BEKI wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi na klabu ya PSV Eindhoven ya Holanzi, Ernstus ‘Ernie’ Wilhelmus Johannes Brandts, ndiye kocha mpya wa Yanga na atawasili wakati wowote kuanzia kesho kusaini mkataba na kuanza kazi.
Mholanzi huyo aliyefukuzwa APR ya Rwanda baada ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Agosti mwaka huu amepewa ukocha wa Yanga, baada ya Mbrazil Marcio Maximo kukataa nafasi hiyo kwa mara ya pili.
Mtaalamu huyo, alizaliwa Februari 3, mwaka 1956 mjini Nieuw-Dijk, Gelderland, mbali na PSV Eindhoven, alichezea pia Roda JC Kerkrade, MVV Maastricht na De Graafschap.
0 comments:
Post a Comment
Toa maoni yako hapa!