StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

September 28, 2012

MSHIKAMANO WAHITAJIKA BAINA YA NCHI ZILIZOENDELEA NA NCHI MASKINI ILI KUMSAIDIA MTOTO WA KIKE KIELIMU

Tweeted this Like this, be the first of your Friends

Mama Kikwete (kulia) akiwa mkutanoni New York nchini Marekani
Na Anna Nkinda – Maelezo, New York
MSHIKAMANO wa pamoja unahitajika baina ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea ili kuhakikisha mtoto wa kike ambaye hajapata nafasi ya kwenda shule anapata elimu, kuwainua wanawake kiuchumi na kupunguza vifo vya kinamama wajawazito na watoto vinavyotokana na tatizo la uzazi na ugonjwa wa kansa.
Hayo yamesemwa jana na Mke wa rais Mama Salma Kikwete wakati akichangia mada kwenye mkutano wa The RAND African First Ladies Initiative uliofanyika makao Makuu ya Taasisi ya Ford mjini New York nchini Marekani.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema kuwa taasisi mbalimbali za Kiserikali na zisizo za kiserikali zinafanya jitihada kubwa ya kuhakikisha kuwa zinawasaidia wanawake wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali za maisha tatizo lililopo ni upungufu wa rasilimai fedha za kuweza kukabiliana na changamoto hizo hivyo basi ushirikiano wa pamoja unahitajika ili kuweza kufanikisha malengo hayo.
Aliendelea kusema kuwa watoto wa kike wakipata elimu ya kutosha watakuwa na silaha muhimu katika maisha yao ya kuweza kupambana na matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na maradhi, ujinga na umaskini kwani elimu ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa lolote Duniani bila ya watu kuwa na na elimu nchi haiwezi kuendelea.
“Ukimuelimisha mtoto hasa mtoto wa kike ambaye amekosa nafasi ya kupata elimu ni faida kwa mtoto, Taifa na Dunia kwa ujumla kwani hivi sasa tumejionea wanawake wengi wakishika nafasi za juu za uongozi kitaifa na Dunia pia wameweza kujikwamua kiuchumi tofauti na miaka ya nyuma”, alisema Mama Kikwete.
Mwenyekiti huyo wa Taasisi ya WAMA alisema kuwa nchini Tanzania watoto wengi wa kike ambao ni yatima na wanaishi katika mazingira hatarishi wameshindwa kupata elimu sawa na watoto wengine hivyo basi aliamua kuanzisha taasisi hiyo ili aweze kuwasaidia watoto hao, kuwainua wanawake kiuchumi na kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto na wanaougua ugonjwa wa kansa kwa kutoa elimu kwa wananchi na vifaa tiba katika vituo vya afya na Hospitali .
Mkutano huo wa siku moja ulihudhuriwa na wake wa marais na wakuu wa Serikali wa Afrika, mke wa rais mstaafu wa Marekani Laura Bush na mke wa waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza Cherie Blair, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na mashirika binafsi kutoka nchi wa Afrika na Marekani.
Katika mkutano huo mambo mbalimbali yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na kuangalia jinsi gani wake wa maraisi na wakuu wa Serikali wanaweza kuleta mabadiliko katika nchi zao katika kuimarisha afya ya mwanamke, kuhakikisha kuwa mtoto wa kike anapata elimu na na kuwainua wanawake kiuchumi pamoja na changamoto wanazoweza kukabiliana nazo

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat