StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

July 28, 2012

Milioni 1.6 wanahitajia msaada wa chakula Zimbabwe

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
Mpango wa Chakula Duniani WFP umetangaza kwamba kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Umoja wa Mataifa na serikali ya Zimbabwe watu milioni 1.6 wanahitajia msaada wa chakula nchini humo mwaka huu. Felix Bamazon Mkurugenzi wa WFP amesema, tayari maafisa wa shirika hilo wameripoti dalili za njaa katika maeneo ya vijijini kutokana na kilimo duni suala lililosababishwa na mvua zisizokuwa na uhakika na ukosefu wa mbegu na mbolea. Suala hilo pia limepelekea Waziri wa Fedha Tendai Biti atabiri kwamba ukuaji wa uchumi wa Zimbabwe utashuka toka asilimia 9.4 hadi asilimia 5.6 mwaka huu wa 2012. Mwezi Disemba pia Ofisi ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa ilisema kuwa watu milioni 1.45 watahitajia msaada wa chakula nchini Zimbabwe.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat