StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

October 30, 2012

Huyu ndiye Binti aliyewagonganisha Ronaldo, Boateng

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
MADRID, HISPANIA
HABARI kutoka Hispania zinasema kuwa Kevin-Prince Boateng amemtaka Cristiano Ronaldo aache kuwasiliana na mpenzi wake, Melissa Satta.

Mwanzoni mwa mwezi huu kulikuwa na habari kwamba nyota wa zamani wa Manchester United, Cristiano Ronaldo ambaye kwa sasa anachezea Real Madrid alikuwa akiwasiliana na mwanamke huyo kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu lengo likiwa ni kumnasa kimapenzi.

Lakini watu wa karibu na Boateng wamesema kuwa mchezaji huyo hajafurahishwa na jambo hilo na amemtaka Ronaldo aache tabia hiyo.

Habari zilizochapishwa katika gazeti la Novella 2000 la Italia zinasema kuwa katika siku za karibuni mchezaji huyo alionekana akiomba namba ya dada huyo.

Cristiano Ronaldo ni mpenzi wa Irina Shayk ambaye amekuwa naye kwa miaka miwili sasa.

Boateng anatarajia kufunga ndoa na Satta mwakani.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat