StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

October 30, 2012

Taarifa rasmi kuhusu Balotelli kumuibukia upya Nicki Minaj

Tweeted this Like this, be the first of your Friends


NYOTA wa Manchester City, Mario Balotelli amepanga kukutana na mwanamuziki Nicki Minaj Ijumaa wiki hii baada ya kushindwa kuonana naye wiki iliyopita.

Mwanamuziki huyo atafanya shoo katika Ukumbi wa MEN Arena Jumaa hii na Balotelli ambaye alilia kukutana naye bila mafanikio, atahakikisha wanaonana.

Habari zinasema kuwa nyota wa Manchester City alitaka kukutana na Nicki Minaj, lakini mwanamuziki huyo alikataa kwa kuwa alikuwa amechoka na pia alikuwa na hasira.

Minaj alitumbuiza katika ukumbi wa News (MEN) Arena wiki iliyopita na Balotelli aliwasili katika shughuli hiyo akiwa na rafiki zake.

Kulikuwa na taarifa kwamba mchezaji huyo alipanga kukutana na nyota huyo kabla ya shoo lakini Minaj aligoma "Mario alisikitishwa na kitendo hicho," alisema mtu wake wa karibu.

Imefahamika kuwa Mario mwenye miaka 21 alikuwa ameandaa kamera kwa ajili ya kumpiga picha dada huyo lakini mambo hayakwenda vizuri.

Balotelli ni nyota katika soka lakini umaarufu huo haukutosha kumtoa ndani Minaj.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat