Tweeted this
Like this, be the first of your Friends

Balozi wa Ubalozi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Tuvako Manongi akizungumza wakati wa mjadala wa wazi ulioandaliwana Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa na kufunguliwa na Katibu Mkuu Ban Ki Moon. Mjadala huo ulihusu uhusiano kati ya Amani na Haki na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai ( ICC) miongoni mwa mambo aliyosisitiza Balozi Manongi ni pamoja na kuishauri ICC kutenda haki bila kuegemea upande wowote na kwamba ijitahidi kujiepusha na ushawishi wa kisiasa kutoka nchi yoyote ile likiwamo Baraza Kuu la Usalama.

Wajumbe wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa katika mkutano wake wa wazi uliokuwa ukijadili uhusiano kati ya Amani na Haki na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai.
Na Maura Mwingira
0 comments:
Post a Comment
Toa maoni yako hapa!