StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

June 27, 2012

VIINGILIO MAONESHO YA SABASABA VYATAJWA

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara Tanzania( TanTrade), imetangaza viingilio vipya vya watu na magari katika maonyesho ya kimataifa ya Sabasaba ambapo watu wazima watalipa Sh 2,500 na watoto Sh 500.

Viingilio hivyo vimeelezwa kuwa vitatumika siku zote isipokuwa siku maalumu ya Juni 7, ambapo viingilio vitakuwa Sh 3,000 kwa watu wazima na watoto Sh 1,000.

Pia, imetangaza viingilio vya magari kuwa tiketi za kupaki magari madogo kila siku ni Sh4,000 na malori ni Sh40,000.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na mdhamini rasmi wa mawasiliano wa maonyesho hayo kampuni ya Vodacom Tanzania,Tan Trade imetangaza kuwa maonyesho hayo yataanza rasmi Juni 28 hadi Julai 8, mwaka huu.

Kwa watakaohudhuria maonyesho hayo na magari madogo watatakiwa kununua tiketi kwa Sh 4,000 kama ambavyo mchanganuo wa malipo unavyobainisha malipo ya huduma nyingine zikiwamo za kupaki magari kama malori na magari makubwa pamoja na huduma nyingine.

Maonyesho ya kimataifa ya Dar es salaam ni maonyesho pekee yanayoongoza katika huduma za masoko Tanzania, maonyesho hayo yanayodumu kwa siku kumi, huvutia watazamaji zaidi ya laki tatu na nusu na kutoa fursa kwa kampuni kuonyesha bidhaa zao na wanaohudhuria kupata nafasi ya kuuliza maswali na kulinganisha ubora wa bidhaaa zilizopo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat