StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

July 13, 2012

Uchumi wa China wapungua kasi ya ukuaji

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
Ukuaji  wa  uchumi  wa  China  umepungua  na  kufikia  kiwango  cha chini  katika  muda  wa  miaka  mitatu  katika  robo  ya  hivi  sasa ya mwaka  huu,  wakati  mauazo  ya  nje  na uwezo wa  watumiaji ukidhoofika. Data  zilizoripotiwa  leo zinaonyesha  kuwa  uchumi  huo wa  pili kwa ukubwa  duniani  umeongezeka  kwa  asimilia  7.6  katika miezi  mitatu  iliyomalizikia  Juni, ikiwa  ni  chini  kutoka  asilimia  8.1 katika  robo  iliyopita  ya  mwaka huu. Huo  ni ukuaji  wa  taratibu mno  tangu  robo  ya  kwanza  ya  mwaka  2009  wakati  mzozo  wa kifedha  duniani ulipokuwa  ukiendelea. Ongezeko  la  bidhaa zinazouzwa  nje  limepungua  taratibu  huku  kukiwa  na  matatizo  ya mahitaji  duniani  na  uwezo  wa  wawatumiaji  nchini  China umedhoofika. Serikali  imepunguza  riba  mara  mbili  tangu mwanzoni  mwa  mwezi  Juni  na  kuanzisha  hatua  kadhaa  za kuchochea  ukuaji  wa  uchumi. Wadadisi  wa  masuala  ya  kiuchumi wanatarajia  ukuaji  wa  uchumi  kurejea  tena  katika  hali  yake  ya kawaida  katika  sehemu  ya  pili  ya  mwaka  huu  lakini  mdororo wa  uchumi unaongeza  kitisho  cha  upotevu  wa  nafasi  za  kazi pamoja  na  kuleta  wasiwasi  wa  kisiasa.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat