StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

July 13, 2012

Matukio ya Kisiasa Africa: Hukumu dhidi ya wanaharakati 24 Ethiopia kutolewa leo

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
Ethiopian students demonstrate outside Addis Ababa Tegbareed Industrial College in the capital's Mexico area., Tuesday, June 7, 2005. Police raided a technical college in Ethiopia's capital Tuesday, beating up students and firing rubber bullets on the second day of defiance of a government ban on demonstrations, witnesses said.  Clashes between police and student demonstrators on Monday left a girl dead, seven people injured and hundreds arrested in protests against disputed election results that left parliament in the hands of the ruling party. (AP Photo)
Nchini Ethiopia leo(13.07.2012) itatolewa hukumu dhidi ya wapinzani na waandishi habari 24. Mwendesha mashaka wa serikali anataka hukumu ya kifungo cha maisha dhidi ya watuhumiwa hao.
Kwa mara nyingine tena inaonekana kuwa serikali ya Ethiopia inakwenda kinyume na haki za binadamu. Ethiopia iliyojitangaza kama "Chui wa Afrika", leo hii inawafungwa wengi wanaharakati, waandishi habari pamoja na wapinzani wa kisiasa.
Wakati chuo kikuu cha mjini Addis Ababa wiki iliyopita kilifanya mahafali yake ya kila mwaka , kutokana na sababu za kiusalama hakuna mpiga picha wa binafsi aliyeruhusiwa, baadhi ya Waethiopia wanatikisa vichwa kutokana na jinsi vyombo vya usalama vinavyoichukulia hali ya mambo nchini humo.
Prime Minister of Ethiopia Meles Zenawi speaks during a panel discussion at the Clinton Global Initiative Annual Meeting, Thursday, Sept. 27, 2007 in New York. (ddp images/AP Photo/Jason DeCrow)

Waziri mkuu wa Ethiopia Meles Zeinawi
Kifungo cha maisha.
Iwapo leo mahakama mjini Addis Ababa itachukua msimamo wa mwendesha mashtaka wa serikali , watahukumiwa waandishi habari pamoja na wanachama wa vyama vya upinzani 24 kifungo cha maisha jela.
Wanashutumiwa kuwa wanaharakati wa chama kinachofanya harakati zake nje ya nchi hiyo cha Ginbot 7, chama ambacho kinaonekana na serikali ya Ethiopia kuwa ni kundi la magaidi. Hali hii inatokana na sheria iliyopitishwa mwaka 2009 ya kupambana na ugaidi, ambapo vyombo vya dola ambavyo vinahusika na ukandamizaji nchini Ethiopia vinapata uwezo wa kuwaandamana watu wanaoikosoa serikali.
Kutokana na kupatikana na hatia mwishoni mwa mwezi Juni, watu hao 24, miongoni mwao akiwemo mwanasiasa wa upinzani Andualem Arage pamoja na mwanablog maarufu Eskinder Nega, serikali ya Ethiopia inaonyesha kwa mara nyingine tena sera zake za kutumia mabavu, kuwa aina yoyote ya ukosoaji utaadhibiwa.
Mwanablog Nega alikamatwa mara baada ya uchaguzi ulioendewa kinyume mwaka 2005, lakini aliendelea kuandika mambo mengi ya kuikosoa serikali katika mtandao wa Internet. Hali hiyo imesababisha sasa kumuingiza matatani.
Laetitia Bader ambaye anafuatilia hali hiyo kwa ajili ya shirika la kutetea haki za binadamu la Human Right Watch akiwa mjini Nairobi amesema.
"Hali ya haki za binadamu iko katika matatizo makubwa , serikali imekuwa ikitumia kila aina ya nyenzo kuzuwia vyombo huru vya habari na haki ya kujieleza na kutoa mawazo. Tuna wasi wasi mkubwa kutokana na ukweli kwamba kati ya watu 34 walioshtakiwa chini ya sheria za kupambana na ugaidi tangu mwaka 2011, kumi na mmoja ni waandishi habari. Kwa hiyo kuna ushahidi kuwa matumizi ya sheria hii ni moja kati ya nyenzo muhimu za kunyamazisha uandishi habari huru na ukosoaji".
Ethiopia kama mtetezi wa Afrika
Ethiopia inajionyesha hivi sasa katika sura mbili tofauti kabisa. Hapa, chui huyu wa Afrika anawavutia wawekezaji kutokana na ukuaji mkubwa wa kiuchumi, ambapo katika mji mkuu Addis Ababa kunachipuka majumba marefu ya ofisi pamoja na mahoteli kila wiki. Hali hii ndio inayompa nafasi waziri mkuu Meles Zenawi kuzungumza kwa niaba ya Afrika katika majukwaa ya kimataifa yanayohusu mazingira, mkutano wa mataifa tajiri na yale yanayoinukia kiuchumi ya G20.
President Barack Obama, center, waves during a family photo at the G20 Summit in Cannes, Thursday, Nov. 3, 2011. Also pictured, first row left to right: Chinese President Hu Jintao; French President Nicolas Sarkozy; Indonesian President Susilo Bambang Yudhoyono. Second row, left to right: Prime Minister Silvio Berlusconi of Italy, German Chancellor Angela Merkel; Prime Minister Recep Tayyip Erdogan of Turkey; Indian Prime Minister Manmohan Singh; Canada Prime Minister Stephen Harper. Top row, left to right: President Khalifa bin Zayed Al Nahyan of the United Arab Emirates; Prime Minister Jose Luis Rodriguez Zapatero of Spain; Prime Minister Meles Zenawi of Ethiopia; Singaporean Prime Minister Lee Hsien Loong; United Nations Secretary General Ban Ki-moon. (Foto:Charles Dharapak/AP/dapd) Meles Zenawi amehudhuria vikao kama hivi vya G20 akiwasemea Waafrika
Katika majukwaa haya anazungumzia upinzani wake dhidi ya ukandamizaji kisiasa, mgawanyiko wa kikabila, ughali wa maisha ulipindukia na hali mbaya ya ukosefu wa ajira kwa vijana.


Haya ndio yaliyosababisha mapinduzi katika mataifa ya Afrika kaskazini.Kwa mara ya kwanza wanaharakati walijaribu kufanya upinzani mwaka 2011 chini ya kauli mbiu inayojulikana kama Beka, kwa lugha ya Kiamhara ikiwa na maana" inatosha". Lakini maandamano yao yalikumbana na vyombo vya dola na kuziliwa katika mtandao wa Internet na facebook.
Mbaya zaidi ni kwamba mataifa fadhili kwa Ethiopia ambayo kati ya mwaka 1991 na 2009 waliipatia nchi hiyo kiasi cha dola za Marekani bilioni 24 kwa misaada ya maendeleo, wananong'ona tu katika ukosoaji wao.
Mwandishi : Ludger Schadomsky / ZR / Sekione Kitojo

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat