StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

July 13, 2012

NIWAZI SASA MYIKA KUKABILIWA NA ADHABU KWA KUSHINDWA KUDHIBITISHA MADAI YAKE DHIDI YA NCHEMBA

Tweeted this Like this, be the first of your Friends

JOHN MNYIKA
NAIBU Spika, Job Ndugai Alhamisi Julai 12, 2012 bungeni alitangaza kuwa Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) atafikishwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge baada ya kushindwa kutoa ushaidi wa kuhusika kwa mbunge wa Iramba Maghaaribi (CCM), Mwigulu Nchemba, katika wizi wa Fedha za Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).
Awali Mwigulu aliomba mwogozo nakusema wiki iliyopita Mnyika alimhusisha na wizi wa EPA uliofanyika wakati yeye (Mwigulu) akiwa chuoni na kiti cha Spika kilimpa Mnyika siku saba kutoa ushahidi dhidi ya tuhuma hizo.
Akitoa mwongozo wake, Ndugai alisema Mnyika alitakiwa apeleke ushahidi wa tuhuma hizo lakini amepeleka maandishi ya utangulizi ila si ushahidi.
“Kwa kuwa siku saba zimepita sasa mwongozo wangu ni…suala hili sasa ninalipeleka katika Kamati ya Haki Maadili na Madaraka ya Bunge, ataandikiwa barua na kamati hiyo ndiyo itakayoshughulikia ushahidi huo,” alisema.
Mapema katika madai yake Mwigulu alisema siku saba alizopewa Mnyika kuthibitisha tuhuma hizo ambazo zililenga kumvunjia heshima kwa chama chake, Watanzania na wapiga kura wake.
“Bunge lako linajua na Watanzania wanajua kwamba wakati tuhuma za EPA zinatokea mimi nilikuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu, nilikuwa bado sijaajiriwa BoT,” alisema.
Baada ya kauli hiyo Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Tundu Lissu, aliomba kiti cha spika (Ndugai), kimwelekeze Nchemba matumizi halali ya mwongozo wa Spika kwa mujibu wa kanuni 68(7), inahusu jambo ambalo limetokea mapema kikao kinachoendelea.
“Sasa mheshimiwa Spika hili jambo ambalo mbunge analizungumzia lilitokea wiki iliyopita, pili kuna maelekezo tayari yaliyotolewa na kiti chako kwamba mheshimiwa Mnyika alete maelezo ya uthibitisho kwa kiti chako na maelekezo yalishatolewa ningefikiri ni jambo la busara kusubiri ofisi yako iseme kama imepata majibu ama haijapata sasa anachotaka huyu anataka mwongozo wa namna gani?” alihoji.
Pamoja na wapenzi wa CHADEMA na MNYIKA kuhoji namna mwongozo wa Ndugai kwa Mwigulu ulivyo shugulikiwa, kwa madai kwamba jambo hilo limetolewa ufafanuzi mapema wakati kuna viporo vingi vya miongozo ya wabunge havijatolewa uamuzi hoja hiyo haitooshi kumuokoa Myika.
Baadhia ya miongozo iliyokaa kwa muda mrefu ni pamoja na madai ya aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kudai kuwa Waziri Mkuu alilidanganya Bunge kuhusu vurugu za Arusha Januari 5 mwaka jana.
Hadi Lema anavuliwa ubunge na Mahakama Aprili mwaka huu, suala hilo lilikuwa halijatolewa uamuzi, huku madai ya mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafuli ya Julai mwaka jana kuwa baadhi ya wabunge wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa waliomba rushwa kwenye halmashauri nayo hadi leo hayajatolea uamuzi.
Lakini pia vipo viporo vya Tundu Lissu dhidi ya William Ngeleja, Kabwe Zitto dhidi ya Mustafa Mkullo na wengine wengi.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat