Martha Mazura (11), mshindi wa shindano la national Book Festival akipiga picha ya pamoja na baba yake mzazi, Bw. Amos M. Cherehani baada ya kupokea tuzo la uandishi bora wa insha lilioandaliwa na the Library of Congress, jijini Washington DC nchini Marekani Jumapili, September 23, 2012 ambapo kati ya washiriki zaidi ya 200, ni washiriki 19 tu ndiyo walioshinda shindano hilo akiwemo Martha ambaye ni Mtanzania pekee kwa mwaka huu kushinda tuzo hilo.
Martha Mazura, Mtanzania aliyeshiriki shindano La uandishi wa insha lilioandaliwa na Library of Congress liitwayo ‘National Book Festival 2012” na kutunukiwa cheti pamoja na zawadi nyingine akipiga picha ya pamoja na waandaaji wa shindano hilo Jumapili, September 23, 2012. Martha ni mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya St. Anthony Catholic School mjini Washington DC.
Martha Mazura akifurahia ushindi wake




0 comments:
Post a Comment
Toa maoni yako hapa!