StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

October 24, 2012

MWANAJESHI AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA NDEGE WAKATI WA MAZOEZI

Tweeted this Like this, be the first of your Friends


Mmoja wa marubani wa jeshi amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa vibaya baada ya ndege waliokuwa wakiirusha kuanguka jijini Dar es Salaam.

Ndege hiyo mali ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWT) ilirushwa na marubani hao wawili na mmoja alifariki dunia wakati akijaribu kuruka baada ya ndege hiyo kupata hitilafu wakati ikiwa hewani.

Tukio hilo limetokea katika kambi ya Jeshi la Anga, Ukonga jijini Dar es Salaam. Mwili wa mwanajeshi aliyefariki umehifadhiwa katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam.

Askari aliyejeruhiwa vibaya katika ajali hiyo ni Kapteni Feruz Kwibika ambaye alipasuka kichwa na kulazwa katika hospitali hiyo. Kwibika alijeruhiwa vibaya baada ya kuruka kutoka ndani ya ndege hiyo kwa lengo la kuokoa maisha yake baada ya kutokea hitilafu hiyo.

Chanzo: http://www.habarimasai.com/

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat