StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

June 26, 2012

SERIKALI YALIA NA SHERIA DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA

Tweeted this Like this, be the first of your Friends WAKATI Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya Duniani leo, waziri wake anayeshughulikia Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi amesema vita dhidi ya dawa za hizo nchini inakwazwa na mkanganyiko wa sheria za kudhibiti uhalifu huo ambao una athari kubwa kwa nguvukazi ya Taifa.

Lukuvi alisema juzi mjini Dodoma kuwa mkanganyiko wa sheria  unagusa mfumo mzima wa uchukuaji wa hatua dhidi ya watuhumiwa kuanzia kukamatwa kwao, maandalizi ya mashitaka husika, kufikishwa mahakamani, vidhibiti walivyokamatwa navyo na hata hukumu zinazotolewa.

Lukuvi ambaye alikuwa akizungumzia maadhimisho hayo ambayo kitaifa yanafanyika leo jijini Dar es Salaam, alisema kutokana na kasoro hizo watuhumiwa wengi wamekuwa wakiachiwa hata baada ya kufikishwa mahakamani.

Alisema Serikali iko kwenye maandalizi ya sheria mpya ambayo pamoja na mambo mengine haitatoa mwanya wa chaguo la hukumu ya faini kwa wale watakaotiwa hatiani na pia haitatoa mwanya wa kutumiwa kwa sheria nyingine kwa makosa ya dawa za kulevya.

“Wataalamu wetu wanatwambia kwamba ziko sheria nyingine kadhaa ambazo zinatumika kuwashtaki hawa watuhumiwa wa dawa za kulevya, sasa ndiyo maana wakati mwingine hata hukumu hazisikiki maana watu wanapigwa faini, wanalipa kisha wanaondoka na kuendelea na biashara hii,”alisema waziri huyo na kuongeza:

“Na hawa vijana wadogo wanaotumiwa kusafirisha, maana kazi ya kusafirisha inafanywa na vijana wadogo tu, wakitumwa wala hawasiti maana wanafahamu kwamba hata wakikamatwa adhabu yao ni faini na mtu wa kulipa faini yupo”.

Alisema mchakato wa kuuhisha sheria hiyo ya dawa za kulevya unaendelea na kwamba Serikali itafanya kila linalowezekana iweze kuwasilishwa bungeni mwaka huu.

Lukuvi alisema mkanganyiko uliopo umekuwa ukikwaza juhudi za serikali za kudhinbiti dawa za kulevya na kutoa mfano wa sheria inayolazimisha kupelekwa madawa ya kulevywa mahakamani kama ushahidi kila wakati hata kama kesi itachukua muda mrefu.

“Hizi dawa zinabadilika, mathalan kama wakati mnamkamata mtuhumiwa zilikuwa na uzito kiasi fulani, kadri zinavyotunzwa uzito unapungua na hata kupata mabadiliko ya kikemikali, hivyo mabadiliko hayo yanafanya dawa hizi zisifae wakati wa kuthibitisha ukweli mahakamani,”alisema.

Kutokana na hilo, alisema ni vigumu kwa binadamu wa kuvumia hadi mwisho kwani wakati mwingine hujikuta katika majaribu ya ama kuiba madawa hayo au kuyatumi lakini pia mahakama kukosesha imani kwani vitu vinavyokamatwa hurudishiwa wahusika wakati sheria inasema vitaifishwe.

“Mfano mahakama Jijini Dar es Salaam iliamuru kuwa mtambo mkubwa uliokuwa umekamatwa urudishwe kwa mhusika jambo ambalo ni hatari kubwa,”alisema.

Alisema vyombo vya sheria ni kama vimekuwa vikikwepa kutumia sheria husika ya dawa za kulevya inayotoa adhabu ya kifungo cha miaka 30 au kifungo cha maisha kwa wanaotiwa hatiani na kwamba sheria mpya itaziba mianya iliyopo.

“Si kwamba nawalaumu mahakimu na majaji kwani wanatumia sheria nyingine zilizopo pia hutegemea mashitaka yamefunguliwa kwa sheria ipi, nakumbuka ni Jaji mmoja tu Nyangarika (Kassim) ambaye aliwahi kutoa hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtuhumiwa mkoani Mtwara, waliobaki ni faini, faini tu,”alisema.

Lukuvi alisema tatizo la dawa za kulevya nchini bado ni kubwa licha ya juhudi mbalimbali za kuwakamata na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa ambao wengi wamekuwa wakiachiwa na ama kesi zao kuchukua muda mrefu bila ya kutolewa hukumu.

Alisema maadhimisho hayo yanafanyika katika kipindi ambacho kumekuwa na ongezeko kubwa la usafirishaji wa kiasi kikubwa cha dawa za kulevya nchini hasa za viwandani zikiwemo heroin na Cocaine.Waziri alitoa mfano kuwa katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Mei, 2012 kilo 234 za heroin zilikamatwa na kuwa kiasi hicho ni kikubwa kukamatwa katika kipindi kifupi.

Lukuvi alisema kuwa ongezeko la dawa za kulevya linaashiria kuwepo ongezeko la matumizi ya dawa hizo nchini, hali ambayo inatishia ongezeko la maambukuzi ya VVU miongoni mwa watumiaji wa dawa hizo.

Kwa mujibu wa Lukuvi, kiwango cha maambuki ya VVU miongoni mwa watumiaji kwa njia ya kujidunga ni asilimia 42 ikiwa ni ytofauti kubwa na kiwango kwa jamii ambacho ni asilimia2012-06-25 5.8.

Lukuvi ambaye aliongozana na baadhi ya wanasheria wa kitendo cha madawa ya kulevya, walisema wakati wowote watatoa pendekezo serikalini kuondoa kigugumizi kwa serikalini ili kila anayekamatwa na kuthibitika kwa maandishi afungwe mara moja.

SOURCE: MWANANCHI
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat