StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

June 26, 2012

WAU SALAAM YA SUDAN KUSINI YA KWANZA KUTHIBITISHA KAGAME CUP

Tweeted this Like this, be the first of your Friends WAKATI Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na kati, Cecafa, likitaraji kuweka hadharani majina ya timu zilizothibitisha ushiriki wake mwaka huu, Wau Salaam ya Sudan ya Kusini imekuwa ya kwanza kuthibitisha ushiriki wake.

Wau inashiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza ikitokea taifa hilo lililopata uhuru wake Septemba 2011 baada ya kujitenga kutoka Sudan Kaskazini.

Michuano ya Kombe la Kagame imepangwa kuanza Julai 14 hadi 28 huku timu 12 zikitarajiwa kushiriki katika mashindano hayo Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Katibu wa Cecafa,  Nicholaus Musonye alisema jana kuwa Juni 24 ilikuwa mwisho wa uthibitisho na leo wataweka rasmi majina ya timu zilizofanikiwa kuthibitisha kabla ya kupanga ratiba hiyo katika droo itakayofanyika mwishoni mwa juma hili Jijini Dar es Salaam.

Musonye alisema mpaka sasa maandalizi yanakwenda vyema huku akiomba wadau wa michezo kusaidia upatikana wa fedha kwa ajili ya timu shiriki ili michuano hiyo ifanyike kwa wakati.

"Tutatangaza timu zote kesho, na timu waalikwa, kwa sasa maandalizi yanakwenda vizuri na tumekuwa tukiwasiliana na waandaaji ambao ni TFF nao wanaendelea vizuri.

"Kikubwa kwa sasa tunaomba misaada kwa wapenzi wa soka kujitokeza katika kuhakikisha mashindano haya yanafanyika kwa wakati," alisema Musonye.

Timu zinazotaraji kushiriki katika michuano hiyo ni pamoja na Tusker ya Kenya, URA (Uganda), APR (Rwanda), Coffee (Ethiopia), Elman (Somalia) na Atletico Olympio ya Burundi.

Nyingine zitakazowania ubingwa unaoshikiliwa na Yanga ni Wau Salaam (Sudan Kusini), Red Sea (Eritrea) Al Hilal (Sudan), Mafunzo (Zanzibar) na wenyeji Tanzania watakaowakilishwa na timu za Simba na Azam.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat