Tweeted this
Like this, be the first of your Friends
WAKATI mwenyekiti wa Simba, Ismail aden Rage akijigamba kulijumuisha
jina la mchezaji Kelvin Yondani katika usajili, habari ambazo millionfortune.com
imezipata, ni kwamba klabu hiyo imeamua kuachana na mchezaji huyo.
Simba
ilikuwa ikihaha kumnusuru beki huyo ambaye amekwishajichomoza Yanga na
hata kuanza mazoezi wakitaka kumrejeshea fedha zake apeleke Yanga na
arudi kundini.
Hatua hiyo ilifikiwa baada ya Yondan kuanza
mazoezi Yanga, na viongozi na wadau wakubwa wa Simba walikuwa katika
hekaheka za kumrudisha kundini.
Awali Habari ambazo Mwananchi
ilizipata zilidai kuwa mdau mmoja wa Simba alikutana na wadau na
viongozi wa Simba pamoja na Yondani mwenyewe wakimshawisi wampatie
fedha, kiasi alichochukua ili azirejeshe Yanga.
Chanzo cha habari
kinasema kuwa wadau na wapenzi wa Simba hawakuridhishwa na hatua ya
beki huyo kwenda Yanga na kwamba anahitajika kwa kiasi kikubwa Simba.
Baada
ya Yondani kuonyesha kuanza mapenzi mapya na Yanga, watu wa karibu wa
Simba wamepitisha azimia la kuachana na beki huyo huku wakiamini kuwa
wachezaji waliopo wanaweza kuvaa viatu vyake.
"Tumeamua kuachana
na Yondani baada ya kumuona Lino Musonda, anacheza vizuri beki wa kati
na tunaamini atatusaidia," kilipasha chanzo hicho.
Kiliendelea
kudai chanzo hicho kuwa, wasiwasi mkubwa ulikuwa beki wa kati lakini
baada ya kupatikana Musonda, kwa pamoja waliridhia beki huyo aende
akacheze soka Yanga.
Wakati hayo yakijiri jana, Mwenyekiti wa
Simba, Ismail Rage alikaririwa na Mwananchi Jumapili akikazia kusema
Yondani amekwenda Yanga kutia mashamsham ya mazoezi lakini bado ni
mchezaji wao halali.
"Yanga wanajifurahisha wenyewe na kelele zao
kamwe hazinitishi...mimi nasema mbivu na mbichi vitajulikana Juni 30
tutakapoweka hadharani kikosi chetu kitakashiriki Ligi Kuu msimu ujao,"
alisema Rage.
Katika hatua nyingine, kocha wa Simba, Milovan
Cirkovic aliyewasili jijini Dar es Salaam juzi usiku akitokea Serbia
alikokuwa kwa mapuziko, anatarajia kuanza mikakati yake leo ya kuinoa
Simba kwa Michuano ya Kagame iliyopangwa kuanza kutimua vumbi Julai 14
mwaka huu.
Kocha huyo pia ataitumia nafasi hiyo kuangalia uwezo
wa wachezaji wapya wa kikosi hicho ambao walisajiliwa na hivi karibuni
bila ya yeye kuwepo licha ya uongozi wa kilabu hiyo kudai kuwa ulikuwa
umepata baraka zake zote.
Kikosi cha mabingwa hao wa Ligi Kuu
ambacho kilikuwa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwa ni sehemu ya
maandalizi ya Michuano ya Kagame.
Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel
Kamwaga alisema kuwa timu hiyo haina muda wa kupoteza kwa sasa na leo
jioni itaendelea na mzoezi yake kwenye Viwanja vya Klabu ya Sigara, TCC,
Chang’ombe, Dar es Salaam.