Gari hilo likiwa mtaroni baada ya kupinduka.
Mwili wa mtoto ukiwa umenasa kwenye gari.
...Mwili huo ukitolewa kwenye gari.
Gari likitolewa katika mtaro huo.
Mtoto aliyenusurika akimlilia mwenzake aliyefariki katika ajali hiyo.
Mtoto na dereva ambao wamenusurika katika ajali hiyo wakiwa na simanzi.
MTOTO mmoja ambaye hakufahamika jina lake, amefariki dunia katika
ajali ya gari eneo la Kigamboni Machava leo wakati gari hilo likitokea
Mji Mwema kuelekea Kivukoni. Ajali hiyo imetokea baada ya gari hilo
lenye namba za usajili T 645 AVG kufunga breki ghafla kutokana na gari
lililokuwa mbele yake nalo kusimama ghafla hivyo kusababisha gari hilo
kuingia mtaroni na kupoteza uhai wa mtoto huyo.
0 comments:
Post a Comment
Toa maoni yako hapa!