Kikosi cha Yanga na Kombe la Kagame |
Na Prince
Akbar
RAIS wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakata Mrisho Kikwete amewapa mwaliko mabingwa
wa Afrika Mashariki na Kati mara mbili mfululizo, Yanga SC kupeleka Kombe lao
Ikulu.
Rais Kikwete |
Mwenyekiti
wa klabu ya Yanga ya Dar es Salaam, Yussuf Mehboob Manji amesema kwamba
wanashukuru kwa mwaliko huo na watakwenda huko, wakirejea kutoka Rwanda ambako
kikosi chao kinakwenda jioni hii.
Manji pia
alisema wanatarajia kufungua tawi la klabu yao nchini Rwanda, kufuatia uhusiano
mzuri uliopo, baina ya klabu hiyo na nchi hiyo kwa pamoja na rais wake, Paul
Kagame.
Manji
alisema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari leo, makao makuu ya klabu
makutano ya mitaa ta Twiga na Jangwani, Dar es Salaam kuhusu mwaliko wa mabingwa
hao Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame kutoka kwa rais wa
Rwanda, Kagame.
Manji akizungumza na wachezaji wa Yanga |
“Tunategemea
kufungua tawi jipya la Yanga nchini Rwanda, hiyo itasaidia kuongeza wanachama
nje ya nchi kwa kuanzia na Rwanda,”alisema Ofisa huyo Mtendaji Mkuu wa Quality
Group Limited.
Yanga itakua
Rwanda kwa wiki moja kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara na wakiwa watacheza mechi tatu za kirafiki dhidi ya Rayon Sports, Polisi na
APR.
0 comments:
Post a Comment
Toa maoni yako hapa!