StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

September 29, 2012

MANISPAA YA ILALA KUWAHUSISHA WANAHABARI NA WAKAZI KATIKA KAMPENI YA USAFI.

Tweeted this Like this, be the first of your Friends


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi akizungumza wakati wa semina ya waandishi wa habari ambapo pamoja na mambo mengine amezungumzia swala la kuweka jiji katika hali ya usafi akisema kuwa Manispaa ya Ilala inakusudia kuingia ubia na wanahabari katika kufanikisha lengo la kuwa Manispaa safi ukizingatia ndio kitovu cha mji wa Dar es Salaam.

Ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kugharamia usombaji wa taka kwani wengi wao wamekuwa wakiona gharama wanazotozwa kwa ajili ya kubeba taka ni kubwa lakini watambue kuwa kwa siku taka zinazokusanywa hufikia hadi tani 1088.



Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini wakimsikiliza kwa makini mkuu wa wilaya ya Ilala wakati akizungumzia mikakati ya Manispaa hiyo kuhakikisha inakuwa mfano wa kuigwa kwa usafi jijini.



Pichani Juu na Chini ni baadhi ya waandishi wa habari wakichangia maoni yao namna ya kuboresha Usafi katika Manispaa hiyo.





Afisa Usafishaji wa Manispaa ya Ilala Bw. Samuel Bubegwa akitoa Elimu kwa wanasemina kuhusiana na jinsi Manispaa hiyo inavyotumia mbinu mbadala baada ya kukusanya taka ambapo huzichambua na kuziweka katika makundi tofauti na nyingine kutumika kuzalishia mbolea ambayo inauzwa na kukuza kipato cha kuendeshea huduma mbalimbali ndani ya manispaa hiyo.



Mwanasheria wa Manispaa ya Ilala Bi. Pamela Mugaruka akielezea matumizi ya sheria ndogo ambazo zimetungwa mwaka 2011 kwa watu wanaozikiuka wakiwemo wanaogoma kulipa ada na kufafanua makosa, adhabu ikiwemo faini zitakazowakabili kwa mujibu wa kifungu cha 17 cha sheria hizo.



Mwenyekiti wa Kata ya Mwenbe Madafu Wifred Kipondya akielezea mafanikio yaliyofikwa na kata yake kutokana na utaratibu waliojiwekea wa kukusanya kodi ambapo sasa wameweza kufikia kukusanya hadi shilingi Milioni 70.



Chati ya mapato na matumizi kwa mwezi kwa mwaka 2009 iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Kata ya Mwembe Madafu Bw. Wifred Kipondya iliyopo ndani ya Manispaa ya Ilala wakati wa semina ya waandishi wa habari.



Baadhi ya maafisa wa Manispaa ya Ilala na waandishi wa habari waliohudhuria semina hiyo leo jijini Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat