StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

September 29, 2012

MGAMBO WATAKA KUWAPIGA WAANDISHI WA HABARI ARUSHA

Tweeted this Like this, be the first of your Friends


wakati sakata la kuwatoa wamachinga jijini Arusha mjini likiendelea waandishi wa habari wamenusurika kugeuzwa mboga na wanamkambo wanaofanya kazi hiyo.


Waandishi hao ambao majina yanaifathiwa ambapo mmoja wapo anatoka katika gazeti la Nipashe na mungine Majira wamenusurika kupigwa pamoja na kuvunjiwa kamera zao wakati walivyokuwa wakiendelea na majukumu yao katika eneo la golden rose jijini Arusha.


Mdau wetu wa libeneke la kaskazini alishuhudia tukio hilo likifanyika wakati waandishi hao wakijaribu kupiga picha wakati mgambo hao wajiji wakiwa wanakusanya vibanda vya wafanya biashara wadogo vilivyokuwa vimewekwa pembezoni mwa barabara.


Mgambo hao wakati waandishi hao wakijaribu kuchukuwa picha hizo za mgambo hao majira ya saa kumi na mbili na nasu jioni mgambo hao waliwavamia na kutaka kuwanyanganya kamera zao ,mara baada ya kupewa amri hiyo na mtu ambaye alikuwa akipita na gari la matangazo akiwasihi machinga kutoa vitu vyao barabarani.

"wakamateni hao waandishi wanaopiga picha wawekeni kwenye gari chukueni na kamera zao "sauti hiyo ilikuwa ikitajwa na mc huyo ambaye alikuwa anatangaza barabarani

Kufuatia tukio hilo lilifanya wananchi wajitokeze kwa wingi na kuanza kuwarushia maneno makali mgambo hao huku wakisema kuwa wanataka kuwafanya kama walivyomfanya mwandishi wa chanel ten


Wakati vurugu hiyo ikiendelea baadhi ya waandishi wa habari walikuja na kuamua tatizo hilo na ndipo mgambo hao wakaondoka mara baada ya kupewa amri na mmoja wa askari aliyekuwa kwenye gari la polisi ambao walikuwa wakiwawanasindikiza gari hilo la mgambo.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat