StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

September 7, 2012

SIRI NZITO ZAFICHUKA KUHUSU KIFO CHA OSAMA, MWANAJESHI ALIYESHIRIKI OPERESHENI HIYO AMEFICHUA

Tweeted this Like this, be the first of your Friends



Wizara ya usalama ya Marekani (Pentagon) imetishia kumpeleka mahakamani mwanajeshi alieandika kitabu kuhusu jinsi yeye na wenzake walivyomuua gaidi Osama Bin Laden aliekua kiongozi wa Al Qaeda.

Mwanajeshi huyo aliekua kwenye kundi la wanajeshi wenye ujuzi wa hali ya juu alikua mtu wa pili kuingia chumbani alipokuepo Osama ambapo kwenye kitabu alichoandika anaeleza kwamba Osama hakua na silaha yoyote walivoingia chumbani kwake, taarifa ambayo inatofautiana na iliyotolewa na Pentagon.

Kanuni zinazoongoza oparesheni kama iliyomuua Osama zinawanyima wanajeshi waliohusika kutoa siri au kutangaza chochote ndio maana anaonekana kavunja makubaliano.

Sasa hivi vyombo vya habari vimeanza kuhusisha hicho kitabu na kampeni za urais jambo ambalo mwanajeshi huyo amelikataa na kusisitiza kwamba amekiandika hicho kitabu ili kuweka hadharani ukweli bila kulenga chama chochote cha siasa wala mgombea.

Matt Bissonnette(36) ambae hafurahii uongozi wa rais Obama, alikua hataki kutambuliwa kwenye vyombo vya habari lakini tayari jina lake limeshajulikana na limesambaa hivyo ilimlazimu kujificha.


HIKI NDO KITABU KINACHOZUNGUMZIA KIFO CHA OSAMA

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat