StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

October 16, 2012

HAFLA KWA AJILI YA WADAU WA MKUTANO WA PPF JIJINI ARUSHA HIVI KARIBUNI ULIOANDALIWA NA BENKI YA CRDB

Tweeted this Like this, be the first of your Friends

Mkurugenzi wa Masoko na Utafika wa benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza katika tafrija iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa PPF jijini Arusha hivi karibuni.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio (wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa PPF,Dk. Adorf Mkenda (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Benki ya CRDB wakati wa hafla ya Mkutano Mkuu wa PPF uliomalizika jijini Arusha hivi karibuni. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Utafika wa benki ya CRDB, Tully Mwambapa, Mkurugenzi wa tawi la Arusha, Chiku Issa, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Saugata Bandyopandyay na Mwenyekiti wa Bodi ya benki ya CRDB, Martin Mmari.


Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio akiwaongoza wageni mbalimbali kupata chakula wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyofanyika jijini Arusha kwa ajili ya wajumbe wa mkutano Mkuu wa PPF ambapo benki ya CRDB ilidhamini tafrija hiyo.

Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Utafika wa benki ya CRDB, Tully Mwambapa, Mkurugenzi wa tawi la Arusha, Chiku Issa wakicheza Rhumba wakati wa hafla ya chakula cha jioni kwa wajumbe wa mkutano Mkuu wa PPF. CRDB ilidhamini hafla hiyo iliyofanyika jijini Arusha.

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Saugata Bandyopandyay (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Masoko na Utafika wa benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kushoto) na Mkurugenzi wa tawi la Arusha, Chiku Issa wakati wa hafla hiyo

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat