Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa nchini
(TPBC) inatambua mkataba (mikataba) kati ya Francis Cheka na Kaike Siyaji
aliyosaini kupigana na Japhet Kaseba siku ya July 7, mwaka huu.
Aidha Kamisheni ya Ngumi za
Kulipwa nchini (TPBC) inamshauri bondia Francsi Cheka awe na mawasiliano mazuri
na promota wa pambano hilo ili hali ya kutoelewana iliyokwisha kujitokeza
imalizwe kwa manufaa ya tasnia ya ngumi nchini.
TPBC inawashauri wadau wote
wanaotaka kufikia makubaliano na mabondia kutofanya hivyo nje ya utaratibu wa
mchezo wa ngumi ambao ni kusaini mikataba mbele ya Kamisheni na wakili ili
maslahi ya wote yalindwe.
Tunapenda pia kuwashauri mabondia
wote kuacha tabia ya kusaini mikataba zaidi ya mmoja hususan wakati bado wakiwa
na pambano mkononi.