StatsCrop - Free website analyzer!

Ads 468x60px

AddToAny

Lorem

Social Icons

June 20, 2012

MWILI WA WILLY EDWARD OGUNDE KUAGWA LEO

Tweeted this Like this, be the first of your Friends
MWILI wa aliyekuwa Mhariri Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Willy Edward Ogunde, unatarajiwa kuagwa leo kuanzia Saa 4:00 asubuhi kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Willy alifariki ghafla usiku wa kuamkia Jumapili mjini Morogoro, baada ya kuanguka kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na maradhi ya moyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya familia ya mzee Edward Ogunde, baada ya mwili huo kuagwa, utasafirishwa kwenda Mugumu, Serengeti, Mara kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika Juni 23, mwaka huu.
“Msiba upo nyumbani kwa kaka yake mkubwa, ndugu Denis Ongiri eneo la Mburahati-Msikitini jijini Dar es Salaam. Mazishi yatafanyika nyumbani kwao kitongoji cha Morotonga, Mugumu, Serengeti,” ilisema Taarifa hiyo.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako hapa!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
 
Web Directories
PageHeat